uk-flag EN

2 Days 1 Night Camping Safari by AfriRoots | Hifadhi ya Nyerere

2 days • 1 night
Pick-up Point: Mlimani City Shopping Complex

About the Safari

Furahia Shangwe la Sikukuu na TANAPA kwa safari ya kipekee ya siku 2 na usiku 1 katika Hifadhi ya Taifa Nyerere kutokea Dar es Salaam. Huu ni wakati wa kupata uzoefu wa kusisimua wa kupiga kambi (camping) katikati ya pori la asili kwa gharama nafuu sana kuliko kulala hotelini.

Usiku wako utapambwa na sauti za viumbe wa porini na anga lenye nyota nyingi, hali inayotoa muunganisho wa karibu na asili.
Siku ya kwanza, utafurahia safari na mandhari ya mtoni Rufiji na game drive ya alasiri, kisha kulala kwenye hema zako salama.
Siku ya pili utamalizia na utalii wa asubuhi kabla ya kurejea Dar es Salaam. Camping inakupa uhuru na kumbukumbu zisizofutika kwa bei rafiki kwa mfuko wako.

2 Days 1 Night Camping Safari by AfriRoots | Hifadhi ya Nyerere

Package Inclusions

  • Usafiri wenye hadhi (4x4 Safari Cruiser au Coaster) pamoja na Dereva/Guide mwenye uzoefu Malipo ya kuingia hifadhini (Park Entry Fees) Game Drive ndani ya Hifadhi kwa muda wote wa siku Chakula cha Mchana (Picnic Lunch) na Maji ya Kunywa Tozo za Serikali na Kodi husika

Package Exclusions

  • Vitu binafsi (kama vile vinywaji vya ziada pombe na ununuzi wa zawadi) Bima ya Afya au Usafiri Zawadi/Ada za Hiari (tips) kwa Dereva na Waongoza Wageni Huduma zisizo kwenye mpangilio wa safari

Itinerary

Siku ya 1 Asubuhi: Kundoka Dar es Salaam kuelekea Hifadhi ya Nyerere mapema, kufika mchana, na kuelekee kambini.

Siku ya 1 Mchana: Kufurahia safari na mandhari nzuri ya kusisimua ya mto Rufiji.

Siku ya 1 Usiku: Kupiga kambi porini, chakula cha jioni, na kufurahia sauti za asili usiku kucha.

Siku ya 2 Asubuhi: Kuamka mapema, kufanya utalii wa asubuhi (game drive), na kisha kuanza safari ya kurejea Dar es Salaam.

Siku ya 2 Mchana: Kuwasili Dar es Salaam jioni.

Available Vehicle(s)

7-seater
🚐 7-seater
Toyota Land Cruiser LC 7SX
TZS 370,000 per person
Remaining Seats: 7 / 7
Book
Link copied to clipboard